WAKATI viongozi wa Ukawa
wakipinga utafiti uliofanywa na TWAWEZA kwa madai ni mbinu chafu iliyotumika
kwa maelekezo ya Kada mmoja wa Chama Cha Mapinduzi mwenye kiu ya kuwania
nafasi ya Urais mwaka 2015,Zitto Kabwe ameupongeza utafiti huo.
nafasi ya Urais mwaka 2015,Zitto Kabwe ameupongeza utafiti huo.
Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge
wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA),japo ana mgogoro na
chama chake hicho aliibuka
chama chake hicho aliibuka
kukubaliana na kuupongeza utafiti huo,na kutoa ushauri tafiti hizo
zifanyike kila baada ya miezi mitatu hadi hapo uchaguzi mkuu utapokapofanyika.
Kabwe ambaye katika
utafiti wa kisiasa uliofanywa na Twaweza alipata asilimia sita kwa watu
wanaofaa kuwania urais kupitia UKAWA, alisema tafiti za kura ya maoni(Opinion
polls) ni muhimu katika demokrasia nchini.
Alisema kitendo kilichofanywa na TWAWEZA ni muhimu sana kwa viongozi wa kisiasa nchini hasa wenye dhamira ya kugombea madaraka katika uchaguzi mkuu ujao kujitathimini baada ya kutambua wanakubalika kiasi gani ndani ya jamii wanayoomba kuiongoza.
Alisema kitendo kilichofanywa na TWAWEZA ni muhimu sana kwa viongozi wa kisiasa nchini hasa wenye dhamira ya kugombea madaraka katika uchaguzi mkuu ujao kujitathimini baada ya kutambua wanakubalika kiasi gani ndani ya jamii wanayoomba kuiongoza.
Aliwapongeza TWAWEZA kwa
kufanya kazi nzuri huku akiwabeza wanaopinga tafiti hiyo,paspo kuleta majibu ya
mbadala na kuwataka kuwa nao wanapaswa kuonyesha utafiti wao unavyosema kwa
sababu utafiti unapingwa kwa utafiti na siyo kwa porojo.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI